UPENDO ASILI YAKE NI MUNGU MWENYEWE!!!!!!!Jamii zetu zimekosa mwelekeo na kuwa na mmomonyoko mkubwa wa maadili kutokana na kukosa upendo. Hii inadhihirishwa na
kuongozeka kwa matendo maovu kila leo katika familia zetu, jamii, kanisa na
hata nchi kwa ujumla.
Kila moja awe mstari wa mbele
kuchukua nafasi yake
ili mambo yaweze kusonga mbele.
MWANAUME NI NANI KATIKA JAMII?
o Mwanaume ni kiongozi
wa familia
o Mwanaume ni mlinzi wa
mwanamke pamoja na familia
o Mwanaume ni mfano wa
kuigwa na jamii
o Mwanaume ni mrithi wa
Mungu
MWANAUME MWENYE ASILI YA MUNGU (MWENYE MAADILI MAZURI)
o Ni mnyenyekevu wakati wote
o Ni mvumilivu wakati wote
o Yupo tayari kusuluhisha kesi yake na
kuanza upya
o Ni mwepesi kusamehe na kusahau
o Ni mtu mwenye utu na anathamini utu wa
mtu
o Anajali watoto na mke wake pia
o Hatakama atakuwa si muaminifu hujitahidi
sana mke wake asijue
MWANAUME MWENYE ASILI YA DUNIA (ASIYE NA MAADILI MAZURI)
o Ni mkorofi kupindukia
o Hana utu wala kujali
o Ni mtu wa lawama wakati wote
o Hana hofu kwa chochote anachokifanya
o Huhesabu makosa wakati wote
o Hana maneno ya faraja kila wakati
hulaani tu
o Hana moyo wa kusamehe, siyo rahisi kesi
yake imalizike kwa amani
MWANAMKE NI NANI KATIKA JAMII?
o Mwanamke ni msaidizi wa mwanaume
o Mwanamke ni taji ya mwanaume
o Mwanamke ni mjenzi wa mji wake na nyumba
yake
o Mwanamke ni kipenzi cha watoto na mume
o Mwanamke ni mwalimu wa familia
o Mwanamke ni mshawishi wa tabia njema kwa
jamii inayomzunguka
MWANAMKE MWENYE ASILI YA MUNGU (MWANAMKE MWENYE MAADILI)
o Hana haraka ya mambo
o Mvumilivu, mnyenyekevu, mtiifu, mkweli,
anaheshima, anajituma, ana utu
o Yupo tayari kufanya suluhu na kusahau
o Yupo tayari kujifunza kutokana na makosa
o Ana mapenzi ya dhati naya ukweli
o Anajali watoto na mume wake pia pamoja na jamii yote
inayomzunguka
o Hayupo tayari kumsaliti mume wake hata kama sababu
zote anazo.
MWANAMKE MWENYE ASILI YA DUNIA (ASIYE NA MAADILI)
o Ni mkorofi
o Hasira zake huwa karibu na za wazi wazi
sana
o Kinywa chake hutoa matusi na lawama
wakati wote
o Hukusanya makosa ya mume wake wakati
wote
o Huwa na upendo wa mtego, hana upendo wa
dhati
o Hupenda kupokea zaidi ya kutoa
o Hulazimisha mambo yafanyike hata kama
haiwezekani kwa wakati huo.
MAPENZI NI NINI?
Kutokana na tafsiri mbali mbali na
mijadala mbali mbali inaonesha mapenzi ni ‘’ mkusanyiko wa hisia za binadamu
zinazopelekea kujenga urafiki wa kudumu kati ya mwanamke na mwanaume au mtu na
mtu mwingine.’’mapenzi asili yake ni Mungu 1Yohana 4;7-8 (7Wapenzi na tupendane, kwa kuwa upendo watoka kwa Mungu. Kila apendaye
amezaliwa na Mungu naye anamjua Mungu.8 Yeye asiyependa hamjui Mungu, kwa
sababu Mungu ni upendo.)
MPENZI NI NANI?
o Ni binadamu aliyejitoa kwa ajili yako,
kusaidiana na wewe katika shida na raha
o Ni mtu yeyote aliyetayari kuumizwa kwa
ajili yako
o Ni binadamu aliye tayari kushauriana na
wewe pale anapoona umekosea
o Ni binadamu aliyetayari kuona
unafanikiwa badala ya kuangauka
o Ni binadamu aliyetayari kushirikisha
hisia zake za kimapenzi na wewe bila kificho
KUFANYA MAPENZI NI NINI?
o Kuonesha hisia zako za kimapenzi kwa
vitendo
o Kufanya vitendo vya upendo kwa wale wote
walio shirikiana na wewe ktika shida au raha
·
Kujitoa kwa jamii nzima zaidi ya kusubiri kupokea Zaidi
KUSUDI LA KUFANYA MAPENZI NI NINI?
o Kumfurahisha mpenzi wako
o Kufurahisha mwili wako na nafsi yako
o Kupata watoto/ kuanzisha familia kwa
kupata watoto
o Kujenga ushirikiano wa kudumu baina yako
na mwenzi wako/ jamii inayokuzunguka
o Kuonesha hisia za mapenzi kwa vitendo na
kufanya suluhu ya matatizo yenu.
MAPENZI YANABEBWA NA VITU VIWILI VIKUBWA AMBAVYO NI:
UPENDO NA HISIA ZA MAPENZI.
UPENDO NI NINI?
Ni tendo la hiari kutoka moyoni mwa mtu
analo kusudia kulifanya kupitia vitendo vya ukarimu, upendo siyo kujivuna, siyo
kujisikia wewe ni bora kuliko wengine, siyo kulipiza kisasi, siyo kulaani bali
kubariki n.k
Upendo ni kusaidiana katika raha na
shida pia kutoa shukurani kwa Mungu na jamii nzima pale unapokuwa umeshirikiana
nao katika jambo lako lolote.
Upendo husaidia kumaliza ugomvi na
kufanya jamii nzima iwe na amani
UKWELI KUHUSU HISIA ZA MAPENZI UPOJE?
o Hisia za mapenzi hujengwa na vitendo vya
upendo
·
Hisia za mapenzi huweza kutoweka na kuhamia mahali
popote pale penye upenyo ambapo vitendo vya upendo hupatikana kwa urahisi. Ili kudumisha
NDOA yenu au mahusiano yenu itakutegemea wewe kama wewe eidha ni mwanamke /
mwanaume. Kwa upande wa mwanamke ana paswa kuonesha upendo zaidi kuliko kupokea.
ISHARA ZA KUTAMBUA (UPENDO WA KIMAPENZI) PENZI LA KWELI.
1.
Mtu huyo atakamata umakini wako na atakuvutia (attention).
2.
Atajaa moyoni na mwazoni mwako kuliko kawaida na wengine.
3.
Utatamani sana uwepo wake wakati wote (kuwa naye).
4.
Utapenda kuwasiliana naye mara kwa mara (kama hamko wote).
5.
Utakuwa na moyo wa kumjali, wema, zawadi na kujitoa sana kwa ajili yake.
6.
Utakuwa na heshima ya juu sana, adabu, utii na uaminifu sana kwake.
7.
Utakuwa na maneno mazuri, maneno laini, na maneno ya upendo kwake.
8.
Utakuwa na moyo/uwezo wa kumvumilia au kuchukuliana naye vile alivyo.
9.
Utakuwa na hamu ya kumgusa au kumshika kwa upendo (si tamaa).
10.
Utakuwa na moyo na utayari wa
kumlinda na kumhifadhi.
11.
Uhusiano wenu utapendeza mbele za watu wengi (si lazima wote)
12.
Utakuwa na amani na furaha ya ajabu moyoni mwako/mwenu.
Mungu alisema kwa mkono wa Mtume Paulo kuuelezea Upendo kwa namna
hii;
1 Cor 13 : 4-8(a)
*
Upendo huvumilia/subira (Love is
patient)
*
Upendo hufadhili/hufanya wema (Love is kind)
*
Upendo hauna husuda (Love doesn’t Envy)
*
Upendo haujivuni (Love is not proud)
*
Upendo haukosi adabu (Love is not rude)
*
Upendo hauna ubinafsi (Love is not selfish)
*
Upendo hauna uchungu (Love is not easily angered)
*
Upendo hauhesabu mabaya (Love doesn’t count wrongs)
*
Upendo haufurahii uovu (Love doesn’t rejoice with evil)
*
Upendo hufurahia ukweli (Love rejoices in truth)
*
Upendo unalinda (love always protects)
*
Upendo huamini yote (Love always trusts)
*
Upendo hutumaini (Love always hopes)
*
Upendo hustahimili (Love always perseveres)
‘’whatever the love you made reflects
your internal feeling and ............................“
Hatuishi
tu kwa kulima na kufuga bali tunalima na kufuga kwa kufuata kanuni za kilimo
bora ili kupata mazao mengi na kufanya kazi zetu kuleta ufanisi mkubwa katika
maisha yetu............nakutakia tafakari njema.
Lakini kumbuka mahusiano mazuri yanahitaji
kufuata misingi yake kwa mipangilio inayokubalika sio bora mapenzi.
Tofautisha
kati ya mapenzi na upendo
Tofutisha
kati ya urafiki na mahusiano
By joseph joachim
No comments:
Post a Comment