Understanding how
agricultural and rural development can create jobs and livelihoods for small
farmers and the landless, while producing food and raw materials for the
SPIRITUAL POWER
Monday, 28 January 2019
THE ORDER OF ENGLISH MASS
THE ORDER OF MASS
INTRODUCTORY
RITE
Priest: In the name of the Father, and of
the Son and of the Holy Spirit.
People: Amen.
Priest: The Lord be with you.
People: And with your Spirit.
Penitential Act
I confess to almighty God, and to you my brothers and sisters, that
I have greatly sinned, in my thoughts and in my words, in what I have done and
in what I have failed to do, through my fault, through my fault, through my most
grievous fault; therefore I ask Blessed Mary ever virgin, all the Angels and
Saints,
Friday, 17 March 2017
*HYDROPONIC FODDER*
MIFUGO BIASHARA!!!
*HYDROPONIC fodder*
Mkombozi pekee wa wafugaji wa ng'ombe, kuku, nguruwe, mbuzi na kadhalika
Mkombozi pekee wa wafugaji wa ng'ombe, kuku, nguruwe, mbuzi na kadhalika
HYDROPONIC ni sayansi/sanaa ya kuotesha mazao bora yenye
tija kwa muda mfupi zaidi bila kutumia udongo kabisa, kwa kutumia maji na virutubisho.
Hydroponic fodder Ni
nzuri zaidi kwa sasa maana Ni nafuu
kulinganisha na vyakula vingine vya mifugo
Hydroponic fodder Ni uoteshaji wa mbegu pasipo kutumia
udongo kwa muda wa siku 5- 7 tu kilo moja ya mbegu za ngano au mtama au shayiri
au Mshindi zinaoteshwa na kumwagiliwa virutubisho maalum na kuongezeka kutoka
kilo moja hadi kilo 10 za CHAKULA cha kuku.
Kwakuwa kuku mmoja hula gram kati ya 100-120gm hivyo kilo moja ya mbegu ikitoa kilo kumi za fodder zinatosha kulisha kuku wakubwa 100 kwa siku Hydroponic fodder Ni CHAKULA cha Mifugo wa aina zote chenye faida nyingi sana.
Kwakuwa kuku mmoja hula gram kati ya 100-120gm hivyo kilo moja ya mbegu ikitoa kilo kumi za fodder zinatosha kulisha kuku wakubwa 100 kwa siku Hydroponic fodder Ni CHAKULA cha Mifugo wa aina zote chenye faida nyingi sana.
FAIDA
ZA CHAKULA CHA HYDROPONIC FODDER KWA MIFUGO
1.Ni nafuu sana kulinganisha na garama za CHAKULA cha madukani au viwandani
1.Ni nafuu sana kulinganisha na garama za CHAKULA cha madukani au viwandani
2.kina virutubisho na vitamini mara 3 zaidi ya CHAKULA cha
kawaida cha Mifugo
3.Hupunguza magonjwa ya mfumo wa hewa kama vile mafua kwa
mfugaji na Mifugo kwani hakina vumbi kabisa.
4.kina protein na Energy/nishati nyingi zaidi mara 3 ya
inayopatikana kwenye vyakula vya kawaida vya Mifugo kama kuku.
5.mifugo hukua haraka sana kutokana na wingi wa protein
ambayo hufanya Kazi ya kujenga mwili na kukua
6.CHAKULA hiki Ni laini sana na kitam kwa kuku na Mifugo
yote (palatable)
6.mmeng'enyo wa chakula hiki huongezeka kutoka 30% kwa
CHAKULA cha kawaida hadi 95% kwa CHAKULA cha hydroponiki hivyo chakula kingi
kutumiwa na mwili wa mifugo na kupunguza kinyesi na usumbufu wa usafisaji banda
7.kinyesi hupungua na kuwa kati ya 5%-10% tu kwani CHAKULA
kingi humeng'enywa na kutumiwa na mwili wa Mifugo
8.mazao kama mayai au maziwa huongezeka kwa 40% kulinganisha
na chakula cha kawaida.
9.kiini cha yai la kuku anayelishwa hydroponic fodder huwa
cha njano sana hata kama Ni kuku wa kisasa
10.Hupunguza garama za ufugaji kwenye manunuzi ya chakula
kwa 50-75% hivyo kuongeza faida.
11.Huhitaji kiasi kidogo cha maji katika kuzalisha
ukilinganisha na vyakula vingine!!!
12.Hupunguza nguvu kazi watu katika kusimamia uzalishaji wa
chakula cha mifugo.
13.Huhitaji eneo dogo kuzalisha chakula kingi
14.Utazalisha kwa wakati kulingana na soko la mifugo husika
15.Haitegemei hali ya hewa unaweza kuzalisha mda wote kwa
vipindi vyote.
1. Fodder growing: https://www.youtube.com/watch?v=2BYvgIlJ2Fo
2. Fodder :
https://www.youtube.com/watch?v=iDQtIjPQni8
3. Hydroponic Fodder :
https://www.youtube.com/watch?v=KE7iSqQ9HIE
Nitafute kwa Namba
0762-96 94 63(WhatsApp)
josejoachim01@gmail.com
Karibuni sana
Natoa elimu na ushauri kwa gharama nafuu naweza kufundisha online au ukaja nilipo/ nifike shambani kwako.
0762-96 94 63(WhatsApp)
josejoachim01@gmail.com
Karibuni sana
Natoa elimu na ushauri kwa gharama nafuu naweza kufundisha online au ukaja nilipo/ nifike shambani kwako.
Usingoje
kesho nitafute Leo ili uweze kufaidika kupitia uwekezaji mdogo tu wa mifugo.
Naweza nikatoa maelekezo online kupitia simu kwa faida yako.
Tuungane kuinua uchumi wa nchi yetu kufikia uchumi kati na viwanda kwa ufugaji wa kisasa usiohitaji gharama kubwa ya malisho!!!
Naweza nikatoa maelekezo online kupitia simu kwa faida yako.
Tuungane kuinua uchumi wa nchi yetu kufikia uchumi kati na viwanda kwa ufugaji wa kisasa usiohitaji gharama kubwa ya malisho!!!
IMEANDALIWA NA JOSEPH JOACHIM- *ANIMAL SCIENTIST*.




Saturday, 1 October 2016
ROZARI YA MAMA BIKIRA MARIA
ROZARI YA MAMA BIKIRA MARIA


MAELEZO YA JUMLA
Anza kusali Rozari kwa kuibusu miguu ya Bwana Yesu katika taswira (picha) yake Msalabani kisha fanya Ishara ya Msalaba (gusisha msalaba huo kwenye paji la so, kifuani, bega la kushoto na kwa kutumia msalaba wa rozari takatifu huku ukiwa unasema “Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina”.
Taja kwa ufupi nia za Rozari hii. Tangaza nia hizo kwa sauti kama mnasali wengi kwa pamoja, Mfano, “Tusali kuombea amani katika nchi yetu na ulimwenguni kote" au tutolee rozari hii kuwaombea wagonjwa wetu: au :tuwaombee wote walioomba tuwaombee" nk. Hiyo ni mifano tu. Au unaweza kutoa mambi kuendana na tendo lililotangazwa kwenye kumi husika la tendo la rozari, au namna nyingine itakayofaa.
Baada ya Sala ya Nasadiki pamoja na ya Baba Yetu, tunamwomba Mungu (Utatu Mtakatifu) fadhila za Imani, Matumaini na Mapendo, zikiambatana na Salamu Maria tatu. Mojawapo ya maneno yafuatayo hutumika:
“Mungu Baba utuongezee Imani. Salamu Maria, …… Mungu Mwana utuongezee matumaini, Salamu Maria, …… Mungu Roho Mtakatifu washa nyoyo zetu kwa mapendo yako, Salamu Maria, …..”
Au;
“Utuongezee Imani ee Bwana, Salamu Maria,…. Utuongezee matumaini ee Bwana, Salamu Maria,…. Uwashe nyoyo zetu kwa mapendo yako ee Bwana, Salamu Maria, …..”
Au;
“Salamu e uliyechaguliwa na Mungu Baba, Salamu Maria,….. Salamu e Mama wa Mungu Mwana, Salamu Maria,….. Salamu e Mchumba wa Mungu Roho Mtakatifu, Salamu Maria,……”
Nk.
SALA ZA ROZARI TAKATIFU
KANUNI YA IMANI
Nasadiki kwa Mungu, Baba Mwenyezi, mwumba mbingu na dunia. Na kwa Yesu Kristu, Mwanaye wa pekee, Bwana wetu; aliyetungwa kwa Roho Mtakatifu, akazaliwa na Bikira Maria, akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato, akasulubiwa, akafa, akazikwa, akashukia kuzimu; siku ya tatu akafufuka katika wafu; akapaa mbinguni; amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi; toka huko atakuja kuwahukumu wazima na wafu. Nasadiki kwa Roho Mtakatifu, Kanisa takatifu katoliki, ushirika wa Watakatifu, maondoleo ya dhambi, ufufuko wa miili, uzima wa milele. Amina.
BABA YETU...
Baba Yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe; ufalme wako ufike, utakalo lifanyike, duniani kama mbinguni. Utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usitutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina
SALAMU MARIA...
Salamu Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote. Na Yesu Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.
ATUKUZWE BABA...
“Atukuzwe Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele, Amina”;
EE YESU WANGU...
Ee Yesu wangu, utusamehe dhambi zetu, utuepushe na moto wa milele, ongoza roho zote mbinguni, hasa za wale wanaohitaji huruma yako zaidi”;
TUWASIFU...
“Tuwasifu milele, Yesu, Maria na Yosef”.
DAMU YA KRISTU..
Damu ya Kristu, iziopoe roho zinazoteseka toharani, izitie nuru ya uzima wa milele. Amina.
Au;
RAHA YA MILELE..
Raha ya milele uwape ee Bwana, na mwanga wa milele uwaangazie. Wapumzike kwa amani. Amina.
NB: Kama muda unatosha uimbwe wimbo wa Bikira Maria japo ubeti mmoja kabla ya kutangaza tendo linalofuata (kila baada ya makumi mamoja)
MATENDO YA ROZARI TAKATIFU
MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)
Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.
Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.
Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara
Tendo la nne; Yesu anatolewa hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.
Tendo la tano; Maria anamkuta Yesu hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.
MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)
Tendo la kwanza; Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.
Tendo la pili; Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.
Tendo la tatu; Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.
Tendo la nne; Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.
Tendo la tano; Yesu anakufa Msalabani. Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.
MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)
Tendo la kwanza; Yesu anafufuka. Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.
Tendo la pili; Yesu anapaa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.
Tendo la tatu; Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.
Tendo la nne; Bikira Maria anapalizwa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.
Tendo la tano; Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.
MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)
Tendo la kwanza; Yesu anabatizwa Mto Jordani. Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
Tendo la pili; Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana. Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.
Tendo la tatu; Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.
Tendo la nne; Yesu anageuka sura. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
Tendo la tano; Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristi. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.
LITANIA YA BIKIRA MARIA
Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie
Kristo utusikie
Kristo utusikilize
Mungu Baba wa Mbinguni, Utuhurumie
Mungu Mwana Mkombozi wa dunia Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja Utuhurumie
Maria Mtakatifu utuombee
Mzazi Mtakatifu wa Mungu utuombee
Bikira Mtakatifu Mkuu wa mabikira utuombee
Mama wa Kristo utuombee
Mama wa neema ya Mungu utuombee
Mama Mtakatifu sana utuombee
Mama mwenye usafi wa moyo utuombee
Mama mwenye ubikira utuombee
Mama usiye na doa utuombee
Mama mpendelevu utuombee
Mama mstajabivu utuombee
Mama wa Muumba utuombee
Mama wa Mkombozi utuombee
Mama wa Kanisa utuombee
Bikira mwenye utaratibu utuombee
Bikira mwenye heshima utuombee
Bikira mwenye sifa utuombee
Bikira mwenye uwezo utuombee
Bikra mweye huruma utuombee
Bikra mwaminifu utuombee
Kioo cha haki utuombee
Kikao cha hekima utuombee
Sababu ya furaha yetu utuombee
Chombo cha neema utuombee
Chombo cha kuheshimiwa utuombee
Chombo bora cha ibada utuombee
Waridi lenye fumbo utuombee
Mnara wa Daudi utuombee
Mnara wa pembe utuombee
Nyumba ya dhahabu utuombee
Sanduku la Maagano utuombee
Mlango wa Mbingu utuombee
Nyota ya asubuhi utuombee
Afya ya wagonjwa utuombee
Kimbilio la wakosefu utuombee
Mtuliza wenye huzuni utuombee
Msaada wa waKristo utuombee
Malkia wa Malaika utuombee
Malkia wa Mababu utuombee
Malkia wa Manabii utuombee
Malkia wa Mitume utuombee
Malkia wa Mashahidi utuombee
Malkia wa Waungama dini utuombee
Malkia wa Mabikira utuombee
Malkia wa Watakatifu wote utuombee
Malkia uliyepalizwa Mbinguni utuombee
Malkia wa Rozari takatifu utuombee
Malkia wa amani utuombee
Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,
Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,
Utusikilize ee Bwana
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,
Utuhurumie.
Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,
Tujaliwe ahadi za Kristo.
Tuombe
Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote; na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.
SALAMU MALKIA...
Salamu Malkia, Mama mwenye huruma, uzima, tulizo na matumaini yetu, salamu. Tunakusihi hapa ugenini sisi wana wa Eva. Tunakulilia tukilalamika na kuhuzunika bondeni huku kwenye machozi. Haya basi, Mwombezi wetu, utuangalie kwa macho yako yenye huruma. Na mwisho wa ugeni huu, utuonyeshe Yesu, mzao mbarikiwa wa tumbo lako. Ee mpole, ee mwema, ee mpendelevu, Bikira Maria.
KUMBUKA...
Kumbuka, ee Bikira Maria mwenye rehema, tokea zamani zote haitambulikani kumeachwa mwenye aliyekimbilia ulinzi wako, mwenye aliyetaka msaada wako, mwenye aliyetaka maombezi yako. Nami nimetumaini kwako, nimekimbilia kwako, ee Mama yangu, Bikira asiye na mfano, nimekuja kwako, nasimama mbele yako mimi mwenye dhambi. Mama wa Neno wa Mungu, usiyachukie maneno yangu, uyapokelee, uyasikilize, ukanifanyizie. Amina.
SALA KWA MTAKATIFU YOSEFU (mwezi wa kumi isaliwe baada ya rozari)
Ee Mt. Yosefu mwenye heri, tunakimbilia kwako katika masumbuko yetu, na kisha omba shime ya Mchumba wako Mtakatifu, tunaomba pia kwa matumaini usimamizi wako. Kwa ajili ya mapendo uliyompenda Bikira Mtakatifu Mzazi wa Mungu, na kwa ajili ya kumtunza Mtoto Yesu, twakuomba sana, utuangalie kwa wema sie tuliokuwa fungu lake Yesu Kristu, tukakombolewa kwa damu yake. Tusimamie katika masumbuko yetu kwa enzi na shime yako.
Ee Mlinzi amini wa jamaa takatifu, uwakinge watoto wateule wa Yesu Kristu. Ee Baba uliyetupenda mno tuepushe na kilema chochote cha madanganyo na upotevu. Ee kinga yetu mwezaji, utusimamie huko juu mbinguni ulipo, tunaposhindana na wenye nguvu wakaao gizani. Kama vile siku za kale ukamwopoa Mtoto Yesu katika hatari ya kuuawa, na leo hivi likinge Kanisa Takatifu la Mungu katika mitego ya adui, na katika shida yote; mtunze daima kila mmoja wetu, tufwate mfano wako, ili tupate na msaada wako, kukaa na utakatifu maisha, kufa kifo chema, na kupata mbinguni makao ya raha milele. Amina.
TUNAUKIMBILIA...
Tunaukimbilia, ulinzi wako, Mzazi Mtakatifu wa Mungu. Usitunyime tukikuomba katika shida zetu, utuokoe siku zote kila tuingiapo hatarini, ee Bikira mtukufu na mwenye baraka. Amina.
Subscribe to:
Comments (Atom)






