Saturday, 1 October 2016

ROZARI YA MAMA BIKIRA MARIA

                  ROZARI YA MAMA BIKIRA MARIA

YESU%20MFALME%20WA%20HURUMA.gif




Rozari%20MBM.png
MAELEZO YA JUMLA
Anza kusali Rozari kwa kuibusu miguu ya Bwana Yesu katika taswira (picha) yake Msalabani kisha fanya Ishara ya Msalaba (gusisha msalaba huo kwenye paji la so, kifuani, bega la kushoto na kwa kutumia msalaba wa rozari takatifu huku ukiwa unasema “Kwa Jina la Baba na la Mwana na la Roho Mtakatifu, Amina”.
Taja kwa ufupi nia za Rozari hii. Tangaza nia hizo kwa sauti kama mnasali wengi kwa pamoja, Mfano, “Tusali kuombea amani katika nchi yetu na ulimwenguni kote" au tutolee rozari hii kuwaombea wagonjwa wetu: au :tuwaombee wote walioomba tuwaombee" nk. Hiyo ni mifano tu. Au unaweza kutoa mambi kuendana na tendo lililotangazwa kwenye kumi husika la tendo la rozari, au namna nyingine itakayofaa.
Baada ya Sala ya Nasadiki pamoja na ya Baba Yetu, tunamwomba Mungu (Utatu Mtakatifu) fadhila za Imani, Matumaini na Mapendo, zikiambatana na Salamu Maria tatu. Mojawapo ya maneno yafuatayo hutumika:
“Mungu Baba utuongezee Imani. Salamu Maria, …… Mungu Mwana utuongezee matumaini, Salamu Maria, …… Mungu Roho Mtakatifu washa nyoyo zetu kwa mapendo yako, Salamu Maria, …..”
Au;
“Utuongezee Imani ee Bwana, Salamu Maria,…. Utuongezee matumaini ee Bwana, Salamu Maria,…. Uwashe nyoyo zetu kwa mapendo yako ee Bwana, Salamu Maria, …..”
Au;
“Salamu e uliyechaguliwa na Mungu Baba, Salamu Maria,….. Salamu e Mama wa Mungu Mwana, Salamu Maria,….. Salamu e Mchumba wa Mungu Roho Mtakatifu, Salamu Maria,……”
Nk.

SALA ZA ROZARI TAKATIFU
KANUNI YA IMANI
Nasadiki kwa Mungu, Baba Mwenyezi, mwumba mbingu na dunia. Na kwa Yesu Kristu, Mwanaye wa pekee, Bwana wetu; aliyetungwa kwa Roho Mtakatifu, akazaliwa na Bikira Maria, akateswa kwa mamlaka ya Ponsyo Pilato, akasulubiwa, akafa, akazikwa, akashukia kuzimu; siku ya tatu akafufuka katika wafu; akapaa mbinguni; amekaa kuume kwa Mungu Baba Mwenyezi; toka huko atakuja kuwahukumu wazima na wafu. Nasadiki kwa Roho Mtakatifu, Kanisa takatifu katoliki, ushirika wa Watakatifu, maondoleo ya dhambi, ufufuko wa miili, uzima wa milele. Amina.

BABA YETU...
Baba Yetu uliye mbinguni, jina lako litukuzwe; ufalme wako ufike, utakalo lifanyike, duniani kama mbinguni. Utupe leo mkate wetu wa kila siku, utusamehe makosa yetu, kama tunavyowasamehe na sisi waliotukosea. Usitutie katika kishawishi, lakini utuopoe maovuni. Amina

SALAMU MARIA...
Salamu Maria, umejaa neema, Bwana yu nawe. Umebarikiwa kuliko wanawake wote. Na Yesu Mzao wa tumbo lako amebarikiwa. Maria Mtakatifu, Mama wa Mungu, utuombee sisi wakosefu, sasa na saa ya kufa kwetu. Amina.

ATUKUZWE BABA...
“Atukuzwe Baba, na Mwana na Roho Mtakatifu, kama mwanzo na sasa na siku zote, na milele, Amina”;

EE YESU WANGU...
Ee Yesu wangu, utusamehe dhambi zetu, utuepushe na moto wa milele, ongoza roho zote mbinguni, hasa za wale wanaohitaji huruma yako zaidi”;

TUWASIFU...
“Tuwasifu milele, Yesu, Maria na Yosef”.

DAMU YA KRISTU..
Damu ya Kristu, iziopoe roho zinazoteseka toharani, izitie nuru ya uzima wa milele. Amina.
Au;
RAHA YA MILELE..
Raha ya milele uwape ee Bwana, na mwanga wa milele uwaangazie. Wapumzike kwa amani. Amina.

NB: Kama muda unatosha uimbwe wimbo wa Bikira Maria japo ubeti mmoja kabla ya kutangaza tendo linalofuata (kila baada ya makumi mamoja)

MATENDO YA ROZARI TAKATIFU

MATENDO YA FURAHA (Jumatatu na Jumamosi)

Tendo la kwanza; Malaika Gabrieli anampasha habari Maria kuwa atakuwa Mama wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie unyenyekevu.
Tendo la pili; Maria Mtakatifu anakwenda kumtembelea Elizabeti. Tumwombe Mungu atujalie mapendo ya jirani.
Tendo la tatu; Yesu anazaliwa Betlehemu. Tumwombe Mungu atujalie moyo wa ufukara
Tendo la nne; Yesu anatolewa hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie usafi wa moyo.
Tendo la tano; Maria anamkuta Yesu hekaluni. Tumwombe Mungu atujalie kuwatii wakubwa wetu.

MATENDO YA UCHUNGU (Jumanne na Ijumaa)

Tendo la kwanza; Yesu anatoka jasho la damu kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie sikitiko la dhambi.
Tendo la pili; Yesu anapigwa kwa mijeledi kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuacha dhambi za uchafu.
Tendo la tatu; Yesu anatiwa miiba kichwani kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kushinda kiburi.
Tendo la nne; Yesu anachukua Msalaba kwa ajili yetu. Tumwombe Mungu atujalie kuvumilia taabu.
Tendo la tano; Yesu anakufa Msalabani. Tumwombe Mungu atujalie kuwapenda Yesu na Maria.

MATENDO YA UTUKUFU (Jumatano na Jumapili)

Tendo la kwanza; Yesu anafufuka. Tumwombe Mungu atujalie kugeuka watakatifu.
Tendo la pili; Yesu anapaa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kwenda mbinguni.
Tendo la tatu; Roho Mtakatifu anawashukia Mitume. Tumwombe Mungu atujalie bidii katika dini yetu.
Tendo la nne; Bikira Maria anapalizwa mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kufa vizuri.
Tendo la tano; Bikira Maria anawekwa Malkia mbinguni. Tumwombe Mungu atujalie kudumu katika njia njema.

MATENDO YA MWANGA (Alhamisi)

Tendo la kwanza; Yesu anabatizwa Mto Jordani. Tumwombe Mungu atujalie uaminifu kwa ahadi zetu za ubatizo.
Tendo la pili; Yesu anageuza maji kuwa divai huko Kana. Tumwombe Mungu atujalie kuukoleza ulimwengu kwa chachu ya enjili.
Tendo la tatu; Yesu anatangaza Ufalme wa Mungu. Tumwombe Mungu atujalie kupokea Ufalme wake kwa toba ya kweli.
Tendo la nne; Yesu anageuka sura. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kuung’arisha ulimwengu kwa uso wa Yesu.
Tendo la tano; Yesu anaweka Sakramenti ya Ekaristi. Tumwombe Mungu atujalie neema ya kujitoa sadaka kwa ajili ya wengine.
LITANIA YA BIKIRA MARIA
Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie
Kristo utuhurumie
Bwana utuhurumie
Bwana utuhurumie
Kristo utusikie
Kristo utusikilize

Mungu Baba wa Mbinguni,                                        Utuhurumie
Mungu Mwana Mkombozi wa dunia                          Utuhurumie
Mungu Roho Mtakatifu                                              Utuhurumie
Utatu Mtakatifu Mungu Mmoja                                 Utuhurumie

Maria Mtakatifu                                                          utuombee
Mzazi Mtakatifu wa Mungu                                       utuombee
Bikira Mtakatifu Mkuu wa mabikira                          utuombee
Mama wa Kristo                                                         utuombee
Mama wa neema ya Mungu                                        utuombee

Mama Mtakatifu sana                                                 utuombee
Mama mwenye usafi wa moyo                                   utuombee
Mama mwenye ubikira                                                utuombee
Mama usiye na doa                                                     utuombee
Mama mpendelevu                                                      utuombee
Mama mstajabivu                                                        utuombee
Mama wa Muumba                                                     utuombee
Mama wa Mkombozi                                                  utuombee
Mama wa Kanisa                                                        utuombee
Bikira mwenye utaratibu                                             utuombee
Bikira mwenye heshima                                              utuombee
Bikira mwenye sifa                                                     utuombee
Bikira mwenye uwezo                                                            utuombee
Bikra mweye huruma                                                  utuombee
Bikra mwaminifu                                                        utuombee

Kioo cha haki                                                              utuombee
Kikao cha hekima                                                       utuombee
Sababu ya furaha yetu                                                            utuombee
Chombo cha neema                                                     utuombee
Chombo cha kuheshimiwa                                          utuombee
Chombo bora cha ibada                                              utuombee

Waridi  lenye fumbo                                                   utuombee
Mnara wa Daudi                                                         utuombee
Mnara wa pembe                                                         utuombee
Nyumba ya dhahabu                                                   utuombee
Sanduku la Maagano                                                  utuombee

Mlango wa Mbingu                                                     utuombee
Nyota ya asubuhi                                                        utuombee
Afya ya wagonjwa                                                      utuombee
Kimbilio la wakosefu                                                  utuombee
Mtuliza wenye huzuni                                                 utuombee
Msaada wa waKristo                                                  utuombee

Malkia wa Malaika                                                      utuombee
Malkia wa Mababu                                                     utuombee
Malkia wa Manabii                                                     utuombee
Malkia wa Mitume                                                      utuombee
Malkia wa  Mashahidi                                                 utuombee
Malkia wa Waungama dini                                         utuombee
Malkia wa Mabikira                                                    utuombee
Malkia wa Watakatifu wote                                       utuombee
Malkia uliyepalizwa Mbinguni                                    utuombee
Malkia wa Rozari takatifu                                          utuombee
Malkia wa amani                                                         utuombee

Mwanakodoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,
Utusamehe ee Bwana.
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye  dhambi za dunia,
Utusikilize ee Bwana
Mwanakondoo wa Mungu uondoaye dhambi za dunia,
Utuhurumie.
Utuombee, Mzazi Mtakatifu wa Mungu,
Tujaliwe ahadi za Kristo.

Tuombe
Ee Bwana Mungu, utujalie sisi watumishi wako afya ya roho na mwili siku zote;  na kwa maombezi matukufu ya Maria Mtakaatifu Bikira daima, tuopolewe na mashaka ya saa, tupate na furaha za milele. Kwa Kristo Bwana wetu, Amina.

SALAMU MALKIA...
Salamu Malkia, Mama mwenye huruma, uzima, tulizo na matumaini yetu, salamu. Tunakusihi hapa ugenini sisi wana wa Eva. Tunakulilia tukilalamika na kuhuzunika bondeni huku kwenye machozi. Haya basi, Mwombezi wetu, utuangalie kwa macho yako yenye huruma. Na mwisho wa ugeni huu, utuonyeshe Yesu, mzao mbarikiwa wa tumbo lako. Ee mpole, ee mwema, ee mpendelevu, Bikira Maria.

KUMBUKA...
Kumbuka, ee Bikira Maria mwenye rehema, tokea zamani zote haitambulikani kumeachwa mwenye aliyekimbilia ulinzi wako, mwenye aliyetaka msaada wako, mwenye aliyetaka maombezi yako. Nami nimetumaini kwako, nimekimbilia kwako, ee Mama yangu, Bikira asiye na mfano, nimekuja kwako, nasimama mbele yako mimi mwenye dhambi. Mama wa Neno wa Mungu, usiyachukie maneno yangu, uyapokelee, uyasikilize, ukanifanyizie. Amina.

SALA KWA MTAKATIFU YOSEFU (mwezi wa kumi isaliwe baada ya rozari)
Ee Mt. Yosefu mwenye heri, tunakimbilia kwako katika masumbuko yetu, na kisha omba shime ya Mchumba wako Mtakatifu, tunaomba pia kwa matumaini usimamizi wako. Kwa ajili ya mapendo uliyompenda Bikira Mtakatifu Mzazi wa Mungu, na kwa ajili ya kumtunza Mtoto Yesu, twakuomba sana, utuangalie kwa wema sie tuliokuwa fungu lake Yesu Kristu, tukakombolewa kwa damu yake. Tusimamie katika masumbuko yetu kwa enzi na shime yako.
Ee Mlinzi amini wa jamaa takatifu, uwakinge watoto wateule wa Yesu Kristu. Ee Baba uliyetupenda mno tuepushe na kilema chochote cha madanganyo na upotevu. Ee kinga yetu mwezaji, utusimamie huko juu mbinguni ulipo, tunaposhindana na wenye nguvu wakaao gizani. Kama vile siku za kale ukamwopoa Mtoto Yesu katika hatari ya kuuawa, na leo hivi likinge Kanisa Takatifu la Mungu katika mitego ya adui, na katika shida yote; mtunze daima kila mmoja wetu, tufwate mfano wako, ili tupate na msaada wako, kukaa na utakatifu maisha, kufa kifo chema, na kupata mbinguni makao ya raha milele. Amina.

TUNAUKIMBILIA...
Tunaukimbilia, ulinzi wako, Mzazi Mtakatifu wa Mungu. Usitunyime tukikuomba katika shida zetu, utuokoe siku zote kila tuingiapo hatarini, ee Bikira mtukufu na mwenye baraka. Amina.

No comments:

Post a Comment